Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Salome Joseph Mbatia
(
27 Disemba
1952
–
24 Oktoba
2007
) alikuwa naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, nchini
Tanzania
.
Mbatia alipata elimu ya msingi katika shule ya St. Anna kuanzia mnamo mwaka
1959
mpaka
1966
.
Aliendelea na masomo ya sekondari katika shule ya St. Joseph mnamo mwaka
1967
hadi
1970
na baadaye kidato cha tano na sita katika shule ya Wasichana ya mjini
Korogwe
(
Tanga
) mwaka
1971
hadi
1972
. Alisomea shahada yake ya kwanza katika
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
kuanzia mwaka
1973
hadi
1976
.
Kati ya mwaka
1982
hadi
1983
alisomea Shahada ya Uzamili kuhusu Menejimenti huko nchini
Marekani
na baadaye akasomea Diploma ya Uzamili katika Utawala na Menejimenti huko nchini
Uholanzi
, hiyo ilikuwa mwaka
1993
.
Aliteuliwa kuwa Naibu Waziri mnamo
Januari
ya mwaka
2006
katika Wizara ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji, kabla ya kupelekwa katika Wizara ya Maendeleo ya Wanawake, Watoto na Jinsia.
Salome Mbatia na dereva wake walikufa baada ya gari walilokuwamo aina ya Nissan Patrol kugongana na gari lingine kubwa aina ya Fuso lililokuwa limebeba mbao eneo la
Kibena
,
wilayani
Njombe
mkoani
Iringa
,
Tanzania
.