Mchoro
wa
uenezi
wa
jenasi
Homo
katika miaka
milioni
mbili
ya mwisho.
Rangi
ya
samawati
Inaonyesha uwepo wa
spishi
fulani
wakati
na
mahali
fulani.
[1]
Ramani ya uenezi wa binadamu ([ka] inamaanisha miaka elfu).
Binadamu
(pia
mwanadamu
) ni
neno
lenye
asili
ya
Kiarabu
linalomaanisha "
Mwana
wa
Adamu
", anayeaminiwa na
dini
za
Uyahudi
,
Ukristo
na
Uislamu
kuwa ndiye
mtu
wa kwanza.
Kisayansi
jina
hilo linaweza kutumika kwa maana ya
Homo sapiens
ili kumtofautisha na
viumbehai
wengine wa
jenasi
Homo
ambao wote walitoweka walau miaka 12,000 hivi iliyopita.
Watu wote walioko leo hii ni
spishi
ileile na tofauti zinazoonekana kati ya
maumbile
yao katika sehemu mbalimbali za
dunia
ni ndogondogo tu.
Utafiti
juu ya
DNA
umethibitisha kwamba binadamu wote wametokana na watu waliokuwepo
Afrika
walau miaka 300,000 hivi iliyopita.
Kwa namna ya pekee,
upimaji
wa
DNA ya mviringo
, ambayo kila mmoja anarithi kwa
mama
tu, umeonyesha kuwa binadamu wote waliopo
duniani
wanachanga mama mmoja aliyewahi kuishi miaka 160,000 hivi iliyopita
[2]
.
Halafu upimaji wa
kromosomu Y
, ambayo kila
mwanamume
anarithi kwa
baba
tu, umeonyesha kuwa wanaume wote waliopo duniani wanachanga baba mmoja aliyewahi kuishi walau miaka 120,000 hivi iliyopita
[3]
, kidogo tu kabla ya watu kuanza kuenea katika
bara
la
Asia
labda kufuatia
pwani
za
Bahari ya Hindi
.
Hata hivyo, miaka hii ya mwisho imegundulika katika baadhi ya wanaume wenye
asili
ya
makabila
ya
Wabangwa
na
Wambo
(
Camerun
,
Afrika ya Kati
) aina ya kromosomu Y tofauti sana na ile ya wanaume wengine wote waliowahi kupimwa, kiasi cha kukadiria zimetofautiana miaka 350,000 hivi iliyopita.
Vilevile, upimaji wa
DNA ya mstari
kwa jumla umeonyesha uwezekano wa kwamba baadhi ya binadamu wa leo, wale wasio wa
Kusini kwa Sahara
, wana
asilimia
1-6 ya
urithi
wa
kibiolojia
kutoka kwa aina nyingine za Homo, hususan
Homo neanderthalensis
, ile ya
pango la Denisova
na ile iliyorithiwa na baadhi ya watu wa
visiwa vya Andaman
(
India
).
Kama hao waliweza kweli kuzaliana na
Homo sapiens
na kuacha
uzao
uliojiendeleza maana yake walikuwa
spishi
moja na yeye. Hapo asili ya binadamu inatakiwa kuhesabiwa ya zamani zaidi sana kuliko miaka 200,000 iliyofikiriwa kwanza
[4]
.
Kutoka bara la Africa watu walienea kwanza
Asia , Australia
na
Ulaya
, halafu
Amerika
toka
kaskazini
hadi
kusini
.
Hatimaye, katika
karne ya 20
watu walikwenda kukaa kwa
muda
katika bara la
Antaktika
kwa ajili ya utafiti.
Ingawa binadamu ana undugu mkubwa wa kibiolojia na
sokwe
na viumbe vingine, ustawi wake hauna mfano, kiasi cha kufanya wengi waamini kwamba tofauti iliyopo inadai kuelezwa kwa uwemo wa
roho
ndani ya
mwili
wake; roho ambayo
dini
hizo
zinasadiki
imetiwa na
Mungu
moja kwa moja.
Kadiri ya
Biblia
, binadamu ameumbwa “kwa mfano wa Mungu” (
Mwa
1:27), mwenye
roho
isiyokufa. Hivyo, Mungu amependa kuwasiliana na watu, akijitambulisha na kujitoa kwetu, tuweze kuishi katika
urafiki
naye na hatimaye tushiriki
heri
yake.
Ameshirikishwa naye ukuu juu ya viumbe vyote vinavyoonekana. “Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota ulizoziratibisha; mtu ni kitu gani hata umkumbuke, na binadamu hata umwangalie? Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu; umemvika taji ya utukufu na heshima” (
Zab
8:3-5). “Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu” (
Yoh
15:15). Amefanya hivyo kwa maneno na matendo yanayoshikamana sana kwa kuwa maneno yanafafanua matendo, nayo matendo yanathibitisha maneno.
Mungu ametufunulia pia
ukweli
juu yetu wenyewe akijibu kabisa maswali yanayotusumbua kuhusu
maana
na lengo la
maisha
yetu. “Mungu hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli” (
1Tim
2:4). “Mungu si mtu, aseme uongo” (
Hes
23:19). Yeye hadanganyiki wala hadanganyi.
Kati ya viumbe vinavyoonekana, mtu tu ni
nafsi
, akiwa na uwezo wa kujifahamu, kujitawala, kujitolea na kupendana na wengine. Basi, anapaswa kulinda hadhi hiyo asitawaliwe na
tamaa
za kila aina. Akifanya hivyo anatimiza mpango wa
Mungu
juu yake na kupendana naye.
Malaika
na watu ndio viumbe pekee vyenye hiari ya kuchagua wenyewe wachangie mpango wa Mungu au la. “Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi, chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako; kumpenda Bwana, Mungu wako, kuitii sauti yake, na kushikamana naye; kwani hiyo ndiyo uzima wako” (
Kumb
30:19-20).
Malaika na watu wanaweza kuchagua hata wawe wema au wabaya
milele
. “Kulikuwa na vita mbinguni: Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni” (
Ufu
12:7-8).
Chaguo letu binadamu linafanyika siku kwa siku kwa kuchukua misimamo mizuri au mipotovu kuhusu
dini
na
maadili
. “Mwayachunguza Maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima” (
Yoh
5:39-40).
Binadamu ni
umoja
wa mambo mawili: roho iliyoumbwa na Mungu moja kwa moja, na
mwili
ulioumbwa naye kwa njia ya
wazazi
.
Maumbile
hayo yanatakiwa kukamilika kwa kupokea na kutimiza
upendo
wa Mungu aliyesema, “’Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi’. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba” (
Mwa
1:26-27).
Hivyo, mwili wetu ni muhimu, kwa sababu umeumbwa na Mungu, umetwaliwa na
Mwanae
ili atuokoe, umehuishwa na
Roho Mtakatifu
atakayeutukuza siku ya
ufufuo
kwa mfano wa Yesu. “Mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili. Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa uweza wake. Je, hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha! Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye?… Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu?” (
1Kor
6:13-16,19).
Utotoni
anasukumwa tu na
haja
za
umbile
lake, ambazo ni muhimu kwake na anazilenga bila ya kuhitaji juhudi.
Lakini akikua anaanza kutambua
tunu
za
maadili
na
dini
, ambazo ni njema, ni muhimu kwa zenyewe na zinamdai azifuate kwa nia imara hadi afikie lengo.
Kwa bidii za kudumu za namna hiyo anamlenga hasa Mungu, wema mkuu.
Anapopitia misukosuko ya
ujana
asikubali kushindwa na
vionjo
wala asikate tamaa, kwa kuwa Mungu amemuumba atawale hata nafsi yake na
mwili
wake.
Mtu wa kwanza kuumbwa na Mungu kadiri ya Biblia alikuwa Adamu, akifuatwa na
Eva
mkewe
. Hapo “Mungu aliona kila kitu alichokifanya, na tazama ni chema sana” (Mwa 1:31).
Hata hivyo, baada ya
dhambi ya asili
anadaiwa bidii katika kutekeleza tunu ili wema alionao uzae matunda.
Basi, apanie kukuza wema aliojaliwa ili kesho awe mtu bora kama
mzazi
,
raia
, kiongozi wa dini na
jamii
n.k.
Penye nia pana njia hata ya kuelekea
utakatifu
utakaokamilika katika
uzima wa milele
.
Binadamu amekabidhiwa na Mungu
dunia
, lakini hasa amekabidhiwa nafsi yake mwenyewe. Itamfaa nini kujua na kutawala
ulimwengu
, asipojijua na kujitawala kweli?
Karne XX
imeleta
maendeleo
makubwa katika
elimunafsia
(=
saikolojia
). Hivyo anaweza kutambua vizuri mema na mabaya yaliyomo ndani mwake.
Lakini akitaka kujifahamu haitoshi asikilize mafundisho hayo au kusoma vitabu vingi juu yake.
Anahitaji kuishi katika
mazingira
bora ambapo ajisikie nyumbani, huru na mtulivu kwa
kupendana
na wenzake, kusikiliza watu wanaomfahamu (hasa walezi wake) wanasema nini juu yake, kujipatia muda wa kutulia peke yake na kujifikiria kulingana na maneno yao, kujichunguza kwa makini kuanzia miaka ya utotoni.
Kwa kuwa
utu
unategemea
urithi
, mazingira na
utashi
wa kila mmoja, anapaswa kuchunguza hayo yote yaliyochangia kumjenga.
Mara kwa mara ajitenge na watu na shughuli ili kutathmini tena maisha yake, kupima
maono
yake na kuweka maazimio ya kufaa, bila ya kusahau kwamba
uhai
wake ni
fumbo
, kwa kuwa unamtegemea Mungu.
- ↑
Stringer, C. (2012). "What makes a modern human".
Nature
.
485
(7396): 33?35.
doi
:
10.1038/485033a
.
PMID
22552077
.
- ↑
Although the original research did have analytical limitations, the estimate on the age of the mt-MRCA has proven robust. More recent age estimates have remained consistent with the 140?200 kya estimate published in 1987: A 2013 estimate dated Mitochondrial Eve to about 160 kya (within the reserved estimate of the original research) and Out of Africa II to about 95 kya.
- ↑
Another 2013 study (based on genome sequencing of 69 people from 9 different populations) reported the age of Mitochondrial Eve between 99 to 148 kya and that of the Y-MRCA between 120 and 156 kya.
- ↑
Omo Kibish Formation and its neighboring sites in Ethiopia have produced some of the earliest examples of fossilised human and australopithecine remains and stone tools.
Richard Leakey
's work there in 1967 found some of the oldest remains of primitive
Homo sapiens
. Earlier believed to be around 125,000 years old, more recent research indicates they may in fact date to c.195,000 years ago. "
The Oldest Homo Sapiens: Fossils Push Human Emergence Back To 195,000 Years Ago
",
ScienceDaily
.
(en)