Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Benjamin Franklin
alizaliwa
mwaka
1706
huko
Boston
. Alikuwa
mwana
wa
kumi
wa fundi wa kutengeneza
sabuni
na
mishumaa
. Baada ya kutumikia kujifunza kwa
baba
yake kati ya
umri
wa miaka 10 na 12, alikwenda kufanya
kazi
kwa
ndugu
yake James,
mchapaji
.
Mnamo
1721
alianzisha
New England Courant
,
gazeti
la
nne
katika
makoloni
. Benyamini kwa
siri
alichangia masomo 14 kwa hilo, na yalikuwa
maandishi
yake ya kwanza yaliyochapishwa.
Mnamo
1723
, kwa sababu ya kuchanganyana na
ndugu
yake, Franklin alihamia
Philadelphia
, ambako alipata
kazi
kama mchapaji. Alitumia mwaka mmoja tu huko na kisha kusafiri kwenda
London
kwa miaka 2 zaidi. Kurudi Philadelphia, alikua kwa haraka katika sekta ya
uchapishaji
.
Alichapisha gazeti la
Pennsylvania
(
1730
-
1748
), ambalo lilianzishwa na mtu mwingine mwaka wa
1728
, lakini mradi wake wa maandishi ya mafanikio zaidi ulikuwa
Poor Richard's Almanac
ya miaka (
1733
-
1758
). Lilipata umaarufu katika makoloni, likiwa la pili tu baada ya
Biblia
, na sifa yake hatimaye ikaenea
Ulaya
.
Alijitolea katika siasa, alikuwa mwakilishi wa bunge lililoongoza vita ya uhuru wa Marekani dhidi ya Uingereza akashiriki kutunga Tangazo la Uhuru wa Marekani na baadaye katiba. Baadaye alisimamia huduma ya posta ya nchi mpya. Alitumwa Ufaransa kama balozi wa Marekani alipofaulu kushawishi serikali ya Ufaransa kujiunga na
Vita ya uhuru wa Marekani
.
Franklin alifanya pia majaribio kuhusu tabia za umeme, mwaka
1752
aliweza kuonyesha kwamba nguvu ya
radi
ni
umeme
akabuni
teknolojia ya kikingaradi
.
|
Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni
mbegu
.
Je, unajua kitu kuhusu
Benjamin Franklin
kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa
kuihariri na kuongeza habari
.
|