Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kamusi Elezo ya Kiswahili
|
Karibu kwenye Wikipedia ya Kiswahili!
Wikipedia
ni mradi wa kuandika
kamusi elezo
kamili na sahihi ya maandishi huru.
Kila mtu anaweza kuhariri makala yoyote, kutoa makosa ya lugha, kutohoa maneno na kuendeleza na kukuza makala, kwa kuandika kwa ufupi au kwa urefu. Tunakushauri ujiandikishe na
kufungua akaunti
. Angalia
Wikipedia:Mwongozo
ili ujifunze unavyoweza kuhariri au kusanifisha ukurasa. Usisite kushiriki; kwa sababu huu ni mradi wa ushirikiano, na hautaisha kamwe. Kamusi elezo itaimarika vizuri zaidi kila wakati. Angalia
ukurasa wa jumuia
,
ukurasa wa jamii
, na ule wa
makala za msingi za kamusi elezo
ili kung'amua unaweza kufanya kazi zipi ili kuboresha Wikipedia.
|
Je, wajua...
|
|
|
|
Makala ya wiki
|
Kassim Said Mapili
(
1937
-
2016
) alikuwa mwanamuziki maarufu wa
muziki wa dansi
kutoka nchini
Tanzania
. Mzee Mapili alizaliwa katika kijiji cha Lipuyu, Tarafa ya Lionya,
Wilaya ya Nachingwea
mkoani
Lindi
mwaka
1937
. Hivyo umauti umekuta Mzee Mapili akiwa na umri wa miaka 79. Alipata elimu ya msingi huko kwao Lipuyu, sambamba na kupata elimu ya dini na mwenyewe aliwahi kusema alianza kupata mapenzi ya kuimba wakati alipokuwa Madrasa akighani
Kaswida
. Mwaka 1958 alijiunga na
White Jazz Band
iliyokuwa na masikani yake huko Lindi.
Mwaka mmoja baadaye akahamia Mtwara na kujiunga na
Mtwara Jazz Band
, lakini mwaka 1962 akajiunga na
Honolulu Jazz Band
ambayo nayo ilikuwa hapo hapo
Mtwara
. Mwaka 1963, Mzee Mapili akachukuliwa na TANU Youth League ya mjini Lindi, na kujiunga na bendi ya
Jamhuri Jazz Band
ya hapo Lindi. Mwaka 1964 Mzee Mapili akachaguliwa kuanzisha bendi ya TANU Youth League ya Tunduru. Mwaka mmoja baadaye alihamia Kilwa Masoko na kujiunga na
Lucky Star Jazz Band
ya mji huo.
?Soma zaidi
|
|
|
Picha nzuri ya wiki
|
TANGAZO LA KIFO cha
Ingo Koll
au
Kipala
kilichotokea tarehe 10, Julai, 2023 nchini Ujerumani. Kipala alikuwa mchangiaji mashuhuri wa Wikipedia kuanzia Disemba 2005 hadi Juni 28, 2023. Siku kumi na mbili mbele tangu kuhariri Wikipedia yetu kwa mara ya mwisho, Mola Jalali Muumba wa mbingu na ardhi, alitwaa kiumbe chake. Kipala atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa wa kuhariri Wikipedia hii. Kwanza akiwa kama msimamizi (admin) baadaye mrasimu (bureaucrat) ambaye ametoa haki za usimamizi kwa wakabidhi ama wasimamizi wengine kama Muddyb, Antoni na wengine wengi tu. Miaka kumi na nane ya kusimamia na kutunga makala mbalimbali itakumbukwa hadi mwisho wa dunia ya Wikipedia. Kipala
amechangia
makala za aina mbalimbali ikiwemo, muziki, filamu, tiba, elimu ya nyota, dini, siasa, demografia, jiografia, sayansi, na mengine mengi. Amepata kuwa msaada mkubwa kwa wachangiaji wapya kutoka sehemu mbalimbali za dunia. Alianzisha Jenga Wikipedia ya Kiswahili kwa lengo la kuboresha makala mbalimbali na kutoa mafunzo kwa watu wapya. Pengo lake halitazibika. Sisi wanajumuia ya Wikipedia ya Kiswahili tunasikitika kutangaza kifo chake!
|
|
Takwimu ya Wikipedia ya Kiswahili
- Idadi ya makala:
80,880
- Idadi ya kurasa zote:
174,502
(pamoja na kurasa za watumiaji, majadiliano, msaada n.k.)
- Idadi ya hariri:
1,334,478
- Idadi ya watumiaji waliojiandikisha:
67,471
- Idadi ya
wakabidhi
:
17
- Idadi ya watumiaji hai:
126
(Watumiaji waliojiandikisha na kuchangia katika muda wa siku 30 zilizopita)
- Bofya hapa kwa kupata namba za sasa
- Katika
mwezi wa Agosti 2020
wikipedia ya Kiswahili iliangaliwa mara milioni 1.73 hivi, ambayo ni sawa na mara 55,800 kwa siku au mara 2,326 kila saa. Asilimia 52 za wasomaji wetu wako Tanzania, asilimia 13 wako Kenya, asilimia 18 wako Marekani na mnamo asilimia 10 wako Ulaya.
- Angalia idadi ya wasomaji kwa makala mbalimbali
- (fungua anwani kwa browser yako, ondoa majina yaliyopo na ingiza jina la makala (hadi makala 10) unayopenda. Unaweza kubadilisha kipindi cha taarifa utakachoona; takwimu kabla ya 2015
hapa
)
- na makala 100 zilizotazamiwa zaidi
"Topviews"
kwa kipindi fulani.
- (unachagua kati ya makala 100 kwa mwezi au kwa siku)
Michango ya wanawiki:
angalia hapa michango ya mtumiaji kwenye kila mradi wa Wikimedia
(
andika jina la mtumiaji kwenye sanduku
)
Jumuia za Wikimedia
Kamusi elezo ya Wiki ni kamusi elezo huru iliyo chini ya
Shirika Lisilo la Kiserikali
la
Wikimedia Foundation
, ambalo linasimamia miradi mingine mbalimbali ambayo imeorodheshwa hapo chini. Mpaka sasa miradi inayopatikana Kiswahili ni Wikipedia na Wikamusi. Wikitabu imewekwa Kiswahili lakini bado ni tupu. Mengine inapatikana Kiingereza pamoja na lugha tofauti.
Wikipedia kwa lugha nyingine
Wikipedia kwa lugha nyingine
|
|