Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Vladimir Semyonovich Vysotsky
(
25 Januari
1938
?
25 Julai
1980
) alikuwa mwimbaji, mwanashairi na mwigizaji katika
Umoja wa Kisovyeti
. Hakukubaliwa na serikali ya siku zake lakini malipendwa sana na watu na hadi leo ana athiri kubwa juu ya wanasanii nchini
Urusi
.
Babake alikuwa mwanajeshi Mrusi wa Kiyahudi, mamake Mrusi.
[1]
Tangu utoto aliwashangaza watu wengine kwa uwezo wake kutunga shairi mara moja, kufanya maigizo na kuimba.
Aliimba tofauti na wote wengine wa siku zake na hakukubali kubanwa na mamlaka ya serikali juu ya utamaduni na sanaa. Aligusa pia mada ambazo hazikukubaliwa na mamlaka ya sanaa ingawa zilikuwa matatizo halisi katika jamii kama vile uhaini, chuki dhidi ya Wayahudi na ukahaba.
Nyimbo nyingi hazikupewa nafasi katika redio au kwenye rekodi za makampuni rasmi kwa hiyo wasikilizaji wake walirekodi wenyewe alipoimba na kusambaza nyimbo kati yao wenyewe kwa njia ya
samisdat
.
Alikuwa pia mwigizaji katika filamu nyingi.
Wikimedia Commons ina media kuhusu: