Anthony Marshon Davis (alizaliwa 11 Machi 1993 ) ni mchezaji wa mpira wa kikapu kutokea Marekani anayeichezea timu ya Los Angeles Lakers katika Chama cha mpira wa kikapu Marekani (NBA).
Davis alikuwa wa kwanza kuchaguliwa mwaka 2012 katika uteuzi wa wachezaji wa Chama cha taifa cha mpira wa kikapu(NBA). Amefanikiwa kuteuliwa katika timu ya mastaa marekani kwa mara sita. Alishinda medali ya dhahabu katika Michezo ya Olimpiki mwaka 2012 akiwa pamoja na timu yake ya Marekani .Mnamo 2021, aliteuliwa katika Timu ya Maadhimisho ya Miaka 75 ya NBA. [1] Davis anazingatiwa sana kama mmoja wa washambuliaji wakuu wa wakati wote. [2]