Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ukataji miti au uondoaji wa misitu
ni kuondolewa kwa msitu kwenye ardhi ambayo inabadilishwa kuwa matumizi yasiyo ya msitu. Ukataji miti unaweza kuhusisha ubadilishaji wa ardhi ya
misitu
kuwa mashamba,
ranchi
, au matumizi ya mijini. Ukataji miti uliokolea zaidi hutokea katika misitu ya
mvua
ya kitropiki. Karibu 31% ya uso wa ardhi wa Dunia umefunikwa na misitu kwa sasa.
Hii ni theluthi moja chini ya eneo la msitu kabla ya upanuzi wa
kilimo
, nusu ya hasara hiyo ilitokea katika karne iliyopita. Kati ya hekta milioni 15 hadi milioni 18 za misitu, eneo lenye ukubwa wa
Bangladesh
, huharibiwa kila mwaka. Kwa wastani miti 2,400 hukatwa kila dakika.