Regina caeli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Antifona ikiimbwa.
Nota za Regina caeli [1]

" Regina caeli " (tamka: re?d?ina ?t?eli; maana yake Malkia wa Mbingu )ni antifona inayotumika kumuelekea Bikira Maria katika Kanisa la Kilatini wakati wa Pasaka , kuanzia Dominika ya Ufufuko wa Yesu hadi Pentekoste .

Katika siku hizo hamsini ndiyo antifona pekee inayotumika kumalizia Sala ya mwisho ya Liturujia ya Vipindi [2] lakini pia inashika nafasi ya sala ya Angelus (inayofanyika mara tatu kwa siku: asubuhi , adhuhuri na jioni ).

Maneno asili kwa Kilatini [ hariri | hariri chanzo ]

  • Regina caeli, laetare, alleluia;
  • Quia quem meruisti portare, alleluia,
  • Resurrexit, sicut dixit, alleluia:
  • Ora pro nobis Deum, alleluia. [3]

Tafsiri ya Kiswahili [ hariri | hariri chanzo ]

  • Malkia wa mbingu, furahi, aleluya;
  • Kwani uliyestahili kumchukua, aleluya,
  • Amefufuka, alivyosema, aleluya:
  • Utuombee kwa Mungu, aleluya. [4]

Historia [ hariri | hariri chanzo ]

Mtunzi wa Regina caeli hajulikani. Kimaandishi inapatikana katika kitabu cha antifona cha mwaka 1200 hivi kinachotunzwa katika Basilika la Mt. Petro , huko Vatikani , jijini Roma . [5]

Tazama pia [ hariri | hariri chanzo ]

Tanbihi [ hariri | hariri chanzo ]

  1. The Regina caeli sung . Youtube. Re-accessed Oct 2021.
  2. "Finally one of the antiphons of the Blessed Virgin Mary is said. In Eastertide this is always the Regina caeli" ( General Instruction of the Liturgy of the Hours, p. 18, paragraph 92 ).
  3. Loyola Press: Regina Caeli . Re-accessed Oct 2021.
  4. Misale ya waamini , toleo la mwaka 2021.
  5. Heinz, Andreas (1997). Walter Kasper (mhr.). Marianische Antiphonen (kwa Kijerumani). Juz. 6 (toleo la 3). Freiburg im Breisgau: Verlag Herder . uk. 1358. ISBN   9783451220012 . Iliwekwa mnamo 15 Oktoba 2021 . {{ cite book }} : |work= ignored ( help ) CS1 maint: date auto-translated ( link )

Viungo vya nje [ hariri | hariri chanzo ]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: