CPU ya Intel
Kichakato kikuu
(pia
Kitengo kikuu cha uchakataji
au
KIU
[1]
; pia:
CPU
,
kifupi
cha
Kiingereza
"
central processing unit
") ni
kichakato
muhimu zaidi ndani ya
tarakilishi
.
Ni kama
ubongo
wa
mashine
hiyo kwa sababu kila sehemu ya tarakilishi inahitajika kwa njia fulani kutekeleza shughuli zake. Kichakato kikuu huwa na
saketi
elektroniki
inayotekeleza maagizo ya
programu
na kupeleka shughuli kwa sehemu nyingine za kompyuta
[2]
.
KIU / CPU ina sehemu tatu ambazo ni muhimu kwa utendakazi wake. Nazo zinaitwa:
- Kitengo cha Hesabu na Mantiki (KIHEMA) (Arithmetic Logic Unit (ALU))
- Kitengo cha Udhibiti (Control Unit)
- Rejesta (Processor registers)
Sehemu hizo zinaunganishwa kwenye
chipu
moja.
[3]
Kitengo cha Hesabu na Mantiki (KIHEMA)
[
hariri
|
hariri chanzo
]
KIHEMA au Arithmetic Logic Unit ni sehemu muhimu ya kichakato kikuu ambayo hushughulikia vitendo vyote vya hesabu, kama vile kujumlisha, kuzidisha, kutoa, kugawanya na hesabu zote za kulinganisha. KIHEMA kina kundi la rejesta ? kumbukizi ziliyojengewa moja kwa moja ndani ya KIU ili kushikilia data inayochakatwa.
[4]
.
Kitengo cha Udhibiti au Control Unit inathibiti amri za programu na kuzituma kwa sehemu nyingine za KIA. Inaratibu vifaa vyote vinavyoingiza na kutoa taarifa mbalimbali katika kompyuta. Vifaa hivi vyaweza kuhusisha skrini, bao bonye, kipanya, printa, na nyinginezo nyingi.
Kwa kawaida kichakato kikuu huhitaji kiasi fulani cha kumbukumbu ambayo hurahisisha uhifadhi wa taarifa mbalimbali mara zinaposubiri nafasi ya kuweza kuwekwa katika hali ya mchakato kuziwezesha taarifa hizo kutoa matokeo yaliyokusudiwa. Sehemu hii ni ya muhimu zaidi kwani hurahisisha kazi ya kichakato kikuu na kuiwezesha kutoa matokeo yaliyokusudiwa kwa muda mfupi kwa kupunguza umbali na muda wa kuzihusisha taarifa mbalimbali wakati wa mchakato
Kichakato kikuu ni kifaa muhimu na chenye gharama kubwa, hivyo utengenezwaji wake ni wa gharama kubwa. Si kila mtu ana uwezo wa kuzitengeneza, hivyo basi ni kampuni chache zenye uwezo wa kukitengeneza. Kampuni hizo zinajumisha Intel, AMD, POWERPC na nyinginezo.
Upatikanaji wa kichakato kikuu unategemea kasi, ukubwa wa mchakato wa data, pamoja na bei na unaweza kuzinunua popote pale kwenye maduka ya spea za kompyuta. Pia unahitajika kujua muingiliano wa kichakato kikuu cha kompyuta unayoitumia na spea utakayoinunua kabla hauja inunua kwani haitaweza kufanya kazi ipasavyo ikiwa kutakuwa na utofauti baina ya
bodi mama
na kichakato kikuu.
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
|
Makala hii kuhusu mambo ya
teknolojia
bado ni
mbegu
.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa
kuihariri na kuongeza habari
.
|