Mpeketoni
ni
mji
wa
Kenya
katika
kaunti ya Lamu
[1]
.
Si mji wa kale bali ulianzishwa katika
miaka ya 1960
kama mradi wa kujenga makazi ya watu na
rais
wa
jamhuri
,
Jomo Kenyatta
.
Kwa asili eneo lilikaliwa na
Wabajuni
lakini wakati wa
uhuru
, na baada ya kuvunjika kwa
Jumuiya ya Afrika Mashariki
, Wakenya wengi walirudi kutoka
Tanzania
hasa
Wakikuyu
, walio sehemu kubwa ya wakazi wa leo, pamoja na
Waluo
na
Wakamba
.
Mashamba
yaliyoanzishwa na
walowezi
hao yanaendelea hadi leo.
Kilimo
ni hasa ya
mahindi
,
pamba
,
muhogo
,
korosho
,
maembe
,
tikiti maji
na
ndizi
.
Kabla ya
ukoloni
wa Kiingereza eneo lilikuwa chini ya
usultani wa Zanzibar
.
Wafanyabiashara
ya watumwa
walitumia njia ya
pwani
kupeleka
watumwa
hadi
Lamu
. Hadi sasa
mwembe
mkubwa unakumbusha mahali ambako misafara ya watumwa ilipumzika na wafungwa walikula maembe na kuacha
mbegu
.
Karibu na Mpeketoni kuna
ziwa Kenyatta
.
Vijiji
ndani ya
tarafa
ni pamoja na Kiongwe, Baharini, Mkunumbi, Bomani, Uziwa, Mapenya, Lakeside, Kibaoni.
Mashambulizi ya al-Shabaab 2014
[
hariri
|
hariri chanzo
]
Tarehe
16 Juni
2014
mji huo ulishambulia na kikosi cha
al-Shabaab
kutoka
Somalia
walioua watu 48. Mnamo saa 3
jioni
waliingia katika mji kwa kutumia
magari
3 wakati wakazi wengi walikuwa wakiangalia
mechi
ya
Kombe la Dunia la FIFA
. Washabaab walitangulia kushambulia
kituo cha polisi
lakini walishindwa kuingia kutokana na upinzani wa
maafisa
. Waliendelea kushambulia
hoteli
, mabaa,
benki
na
ofisi
za
serikali
ilhali walifyatulia
risasi
hovyo wananchi waliowaona pamoja na
watoto
wadogo na wakinamama.
[2]
Baada ya saa sita
usiku
waliondoka tena lakini njiani waliua wananchi wengine, kwa mfano watu sita huko Kibaoni.
- www.wimvandenburg.nl. shirika la Kiholanzi linalotoa misaada kwa miradi katika Mpeketoni
| Makala hii kuhusu maeneo ya
Kenya
bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu
Mpeketoni
kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa
kuihariri na kuongeza habari
.
|