Wasiosadiki Utatu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Wasiosadiki Utatu ni Wakristo ambao wanakusha fundisho hilo la msingi la madhehebu karibu yote ya dini iliyoanzishwa na Yesu .

Biblia haitumii neno Utatu , ambalo limetungwa na wanateolojia katika jitihada za kufafanua ukweli wa Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu na wa Roho Mtakatifu .

Kwa kuwatambua wote wawili kuwa wa milele lakini si Baba , wanateolojia wengi, hasa ma babu wa Kanisa , walikiri kuwa zote tatu ni nafsi tofauti za Mungu pekee.

Mitaguso ya kiekumene kuanzia karne ya 4 ilithibitisha mafundisho hayo kama imani sahihi na kutupilia mbali yaliyo kinyume kama uzushi . [1] [2] [3] [4]

Hata hivyo Waario na wengineo hawakukubali dogma hizo, [5] hivyo asilimia ndogo ya Wakristo imeendelea kukataa kusadiki fumbo la Utatu, na kukiri umoja wa nafsi ya Mungu, [6] [7] [8] [9] ingawa kwa kutofautiana wao kwa wao. [10]

Kati ya makundi makubwa zaidi yenye msimamo huo kuna Wamormoni na Mashahidi wa Yehova , lakini pia baadhi ya Wapentekoste .

Tanbihi [ hariri | hariri chanzo ]

  1. Roger E. Olson, Christopher Alan Hall (Eerdmans 2002 ISBN 978-0-80284827-7), p. 15
  2. Roger E. Olson, The Story of Christian Theology (InterVarsity Press 1999 ISBN 978-0-83081505-0), p. 173
  3. Bernhard Lohse, A Short History of Christian Doctrine (Fortress Press 1966 ISBN 978-1-45140423-4), p. 55
  4. Deno John Geanakoplos, Constantinople and the West (University of Wisconsin Press 1989 ISBN 978-0-29911884-6), p. 152
  5. Frank Leslie Cross, Elizabeth A. Livingstone (editors), The Oxford Dictionary of the Christian Church (Oxford University Press 2005 ISBN 978-0-19280290-3), entry: "Arianism"
  6. http://www.britannica.com/EBchecked/topic/590747/Theodosius-I
  7. http://www.fourthcentury.com/index.php/urkunde-33
  8. "Nakala iliyohifadhiwa" . Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2013-10-14 . Iliwekwa mnamo 2014-09-22 .
  9. http://www.britannica.com/EBchecked/topic/12976/Albigensian-Crusade
  10. von Harnack, Adolf (1894-03-01). "History of Dogma" . Iliwekwa mnamo 2007-06-15 . [In the 2nd century,] Jesus was either regarded as the man whom God hath chosen, in whom the Deity or the Spirit of God dwelt, and who, after being tested, was adopted by God and invested with dominion, (Adoptionist Christology); or Jesus was regarded as a heavenly spiritual being (the highest after God) who took flesh, and again returned to heaven after the completion of his work on earth (pneumatic Christology)

Marejeo [ hariri | hariri chanzo ]

Viungo vya nje [ hariri | hariri chanzo ]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu .
Je, unajua kitu kuhusu Wasiosadiki Utatu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari .