Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ushairi
ni
utungo
wa
kisanaa
ulio na madhumuni ya kutumbuiza au kuelimisha. Tena, ushairi ni
tawi
mojawapo la
fasihi andishi
. Kinyume chake ni
nathari
.
[1]
Inawezekana kutunga
mashairi
yenyewe au kutumia
lugha ya kishairi
katika aina nyingine za sanaa, kwa mfano
tamthiliya
au
nyimbo
.
Ushairi una
historia
ndefu. Kwa mfano,
mwanafalsafa
Aristotle
katika
kitabu
chake
Ushairi
("Poetics" kwa
Kiingereza
) anachunguza matumizi yake katika
hotuba
, tamthiliya, nyimbo na
futuhi
.
Ushairi una vipera vifuatavyo:
1. nyimbo
2. ngonjera
3. mashairi mepesi
4. maghani
5. tendi
6. rara
7. rara nafsi
Maana na tafsiri ya ushairi kulingana na washairi wakubwa
[
hariri
|
hariri chanzo
]
Katika kujenga hoja mbalimbali za ushairi ni nini. Wakongwe na magwiji wa ushairi wa awali walieleza maana mbalimbali za ushairi kulingana na utunzi. Wakongwe hao waliamini kuwa mtunzi ana uhuru wa kutunga aina za mashairi wazipendazo bora tu wapashe ujumbe kwa hadhira. Washairi hao walitunga mashairi bila kujali arudhi za ushairi.
[2]
Ushairi ni sanaa ya vina inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi. Zaidi ya kuwa sanaa ya vina, una ufasaha wa maneno machache au muhtasari. Mwauliza wimbo, shairi na tenzi ni nini? Wimbo ni shairi ndogo, ushairi ni wimbo mkubwa na utenzi ni upeo wa ushairi. Mwauliza tena kina na ufasaha huweza kuwa nini? Kina ni mlingano wa sauti za herufi. Kwa maneno mengine huitwa mizani ya sauti na ufasaha ni uzuri wa lugha. Mawazo na maoni na fikra za ndani zinapoelezwa kwa muhtasari wa shairi huvuta moyo kwa namna ya ajabu.
Ushairi ni lafudhi ya asili inayoeleweka zaidi na moyo wa kila mtu anayeishi katika jamii inayohusika.
“Ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale. Ndicho kitu kilicho bora sana katika maongozi ya dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha nzito yenye kunata iliyopangwa kwa urari wa mizani na vina maalumu kwa shairi.
Utungo ambao katika kila ubeti wake kuna ulinganifu wa vina vitukufu vilivyopangwa kimoja baada ya chenziye; wenye vipande vilivyo na ulinganifu wa mizani zisizo pungufu wala zilizo zaidi; na vipande hivyo viwe vimetandwa na maneno ya mkato maalum na yenye lugha nyofu, tamu na laini, lugha ambayo ni tetelezi kwa ulimi kwa kuitamka, lugha ambayo ina uzito wa fikra, tamu kwa mdomo wa kuisema, tumbuizi kwa masikio ya kuisikia na yenye kuathiri moyo uliokusudiwa na kama ulivyokusudiwa.
Uandishi wa mashairi ya Kiswahili ulianzia Lamu na Pate kabla ya kuenea katika Mkoa wa Tanga, Zanzibar, na maeneo mengine ya jirani. Utamaduni huo bado unatekelezwa hadi leo
[3]
|
Makala hii kuhusu mambo ya
lugha
bado ni
mbegu
.
Je, unajua kitu kuhusu
Ushairi
kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa
kuihariri na kuongeza habari
.
|