Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Umri wa Kati
(pia:
makamo
) ni kipindi cha
maisha
baada ya
ujana
lakini kabla ya
uzee
. Majaribio mbalimbali yamefanywa kufafanua
umri
huu, ambao uko katika
robo
ya
tatu
ya
wastani
cha kuishi kwa
binadamu
[1]
.
Watu wazima
wenye umri wa kati mara nyingi huonyesha
ishara
za kuzeeka kama vile
ngozi
kutokuwa nyororo na
nywele
iliyo na
mvi
.
Nguvu
pia hupungua, na kilo 5-10 kg (10-20 lb) ya mafuta ya mwili, kupunguza upumuaji na upungufu katika upigaji wa moyo. Hata hivyo, watu huzeeka kwa viwango tofauti na kuna tofauti kubwa inaweza kuwa kati ya watu wa rika.
[2]
Uzazi
wa wote wawili,
mwanamume
na
mwanamke
, hupungua kwa umri. Kuwa
mjamzito
unapozeeka huongeza hatari na
mtoto
kuzaliwa na baadhi ya matatizo kama vile
ugonjwa wa Down
. Uzazi katika umri mzee pia huongeza hatari ya kupoteza mtoto au kasoro nyingi, ikiwa ni pamoja na
skizofrenia
,
autism
, upungufu wa akili na
bipolar
.
[3]
[4]
[5]
[6]
Wanawake wengi hupitia kikomo cha kuzaa katika umri wao wa mwishoni wa miaka ya 40 au 50.
[7]
Viwango vya utasa miongoni mwa wanaume pia huongezeka wanapozeeka , na kikomo katika umri wa 45.
[8]
Katika
nchi zilizoendelea
, vifo huanza kuongezeka kuanzia umri wa 40 na kuendelea, hasa kutokana na matatizo ya afya yanayohusiana na umri kama vile
ugonjwa wa moyo
na
kansa
.
[9]
[10]
Hata hivyo, wengi wa umri wa kati katika nchi zilizoendelea hutarajia kuishi katika
uzee
.
Matarajio ya kuishi
katika
nchi zinazoendelea
yako chini na hatari ya kifo katika miaka yote iko juu zaidi.
[9]
- ↑
Kulingana na kamusi ya Collins, "... kipindi hiki kwa kawaida huwa kati ya 40 na 60".
OED
huwa na ufafanuzi sawa lakini huanzia baadaye, "... kipindi kati ya ujana na uzee, kati ya 45-60". Sensa ya Marekani huorodhesha umri wa kati ukijumuisha kundi la umri wa 35-44 na 45-54, wakati
mwanasayansi
mashuhuri wa kijamii,
Erik Erikson
, alionelea kuwa umri huo ulikwisha baadaye kidogo na kufafanua umri wa kati ukiwa kati ya 40 na 65.
- ↑
Shephard, Roy J. (7 Machi 1998).
"Aging and Exercise"
.
Encyclopedia of Sports Medicine and Science
. T.D.Fahey
. Iliwekwa mnamo
2007-06-26
.
- ↑
Heubeck, MA, Elizabeth (2005-06-29).
"Age Raises Infertility Risk in Men, Too: Risks associated with men's biological clocks may be similar to women's"
.
WebMD
. MedicineNet
. Iliwekwa mnamo
2009-10-16
.
- ↑
"Miscarriage significantly associated with increasing paternal age"
. Columbia University's Mailman School of Public Health. 2006-08-03
. Iliwekwa mnamo
2009-10-16
.
- ↑
Raeburn, Paul (Februari/Machi 2009).
"The Father Factor: Could becoming a father after age 40 raise the risks that your children will have a mental illness? (PDF)"
(PDF)
.
Scientific American Mind
: 30?33
. Iliwekwa mnamo
2009-10-16
.
;
- ↑
Cannon, Mary (2009-03-10).
"Contrasting Effects of Maternal and Paternal Age on Offspring Intelligence"
. Public Library of Science
. Iliwekwa mnamo
2009-10-16
.
- ↑
"Vidokezo vya matibabu katika BBC"
. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka
chanzo
mnamo 2009-03-19
. Iliwekwa mnamo
2010-01-29
.
- ↑
Cannon, Mary (2003-06-26).
"Male Biological Clock is Ticking, Too"
.
WebMD Health News
. Iliwekwa mnamo
2009-10-16
.
- ↑
9.0
9.1
"Life Expectancy Profiles"
. BBC. 6 Juni 2005
. Iliwekwa mnamo
2007-06-26
.
- ↑
"UK cancer mortality statistics by age"
. Cancer Research UK. 2007
. Iliwekwa mnamo
2007-06-26
.
- Kamusi la Hisia la Collins Toleo la nne 1999 Collins (en chapisho la Harper la wachapishaji wa Collins ) Glasgow
ISBN 0004722574