Muungano wa Mashirikisho ya Soka Barani Ulaya
(
kifupi
:
UEFA
kutoka
Kifaransa
:
Union des associations europeennes de football
) ni chama kinachotawala na kudhibiti
kandanda
barani Ulaya.
UEFA inawakilisha mashirikisho ya soka ya mataifa ya
Uropa
, inaendesha mashindano ya mataifa na ya vilabu barani Uropa, na inadhibiti pesa za tuzo, kanuni na haki za vyombo vya habari katika mashindano hayo. Mashirikisho kadhaa ya kitaifa ambayo kijiografia yako barani
Asia
au mara nyingi katika
Asia
huwa katika UEFA na wala sio katika
Shirikisho la Soka la Asia
(AFC). Mataifa haya ni
Armenia
,
Georgia
,
Kazakhstan
,
Uturuki
,
Israeli
,
Kupro
,
Urusi
na
Azerbaijan
(Israeli na AFC Kazakstan ni wanachama wa zamani wa AFC). Cyprus ilichagua kuorodheshwa kama taifa la soka ya Uropa - ilikuwa na chaguo la Ulaya, Asia au Afrika.
UEFA ndilo shirikisho la bara kubwa zaidi katika
FIFA
kwa sita yaliyomo. Kati ya mashirikisho yote, kwa mbali ndilo lenye nguvu zaidi katika masuala ya mali na ushawishi katika ngazi ya klabu. Karibu wachezaji wote mashuhuri wa soka ulimwenguni hucheza katika ligi za Uropa, kidogo kwa sababu ya mishahara inayopatikana kutoka vilabu tajiri zaidi duniani, hasa katika
Uingereza
,
Uhispania
,
Italia
na
Ujerumani
. Nyingi ya timu za kitaifa zenye nguvu zaidi duniani ziko katika UEFA. Katika nafasi 32 zilizoko katika
Kombe la Dunia la FIFA
2010, 13 zilitengewa timu za mataifa ya UEFA, na kwa sasa 12 ya timu bora 20 kulingana
Orodha ya FIFA
ya Dunia ni wanachama wa UEFA.
UEFA ilianzishwa tarehe 15 Juni 1954 mjini
Basel
, Uswisi kufuatia majadiliano kati ya mashirika ya soka ya
Ufaransa
,
Italia
na
Ubelgiji
. Makao makuu yalikuwa Paris hadi 1959 wakati shirikisho hili lilihamia
Bern
.
Henri Delaunay
ndiye aliyekuwa Katibu Mkuu wa kwanza na
Ebbe Schwartz
rais. Ofisi ya utawala wake imekuwa katika
Nyon
, Uswisi, tangu mwaka 1995. Awali ilikuwa inajumuishwa na vyama 25 vya kitaifa. Hivi sasa kuna vyama 53 (angalia chini ya ukurasa huu au
Orodha ya UEFA timu za kitaifa za kandanda).
Timu za UEFA za kitaifa zimeshinda
Kombe la Dunia la FIFA
mara tisa (Italia 4, Ujerumani 3, Uingereza na Ufaransa nyara kila moja), kama timu za mataifa ya
CONMEBOL
, na vilabu vya UEFA vimeshinda
Kombe
la
intercontinental
mara 21 na
Kombe la dunia la Klabu la FIFA
mara 3, kombe moja tu chini ya vilabu vya CONMEBOL.
UEFA, kama mwakilishi wa vyama vya kitaifa, imekuwa na mifarakano kadhaa na
Tume
ya
Ulaya
. Katika miaka ya 1990 masuala ya haki za televisheni na hasa uhamisho wa kimataifa (
tawala la Bosman
) umebidi upitie baadhi ya mabadiliko makubwa ili kubakia sambamba na sheria ya Ulaya.
Mashindano makuu ya timu za wanaume za kitaifa ni ya
Mabingwa wa Soka ya Uropa ya UEFA
, yaliyoanza mwaka 1958, na fainali ya kwanza ikafanyika mwaka 1960, na ikajulikana kama Kombe la Mataifa ya Ulaya hadi 1964. UEFA pia inaendesha mashindano ya kitaifa ya walio na miaka
Chini ya 21
,
Chini ya 19
na
Chini ya 17
. Kwa timu za taifa za wanawake, UEFA huendesha
Michuano ya Wanawake ya UEFA
kwa pande mwandamizi za kitaifa na
Mabingwa chini ya 19
katika kiwango cha miaka chini ya 19, tangu mwaka 2008 kuna
Kombe la UEFA la Chini-17
kwa walio na chini ya miaka 17.
UEFA pia hupanga
Kombe la UEFA-CAF Meridian
na
CAF
kwa timu za vijana.
UEFA ilizindua
Kombe la Kanda la UEFA
, kwa timu zisizo na utaalamu, mwakani 1999.
Katika
futsal
kuna
michuano
ya
UEFA Futsal
na
Michuano ya UEFA Futsal Chini ya 19
.
UEFA pia huendesha mashindano mawili makuu ya vilabu barani Ulaya (yajulikanayo kama
mashindano ya vilabu ya UEFA
:
Ligi ya Mabingwa ya UEFA
ilifanyika kwanza mwakani 1955, na ilikuwa ikijulikana kama Kombe la Vilabu Bingwa barani Uropa (au Kombe la Uropa tu) hadi 1992; na
Ligi ya Uropa ya UEFA
(awali Kombe la UEFA), kwa washindi wa mchujo wa kitaifa na timu za ligi bora zaidi, ilizinduliwa na Uefa mwaka 1971 kama mwandamizi wa
Kombe la Inter-Cities Fairs
(pia ilianza mwaka 1955 lakini haikutambuliwa na UEFA
[1]
Shindani la tatu,
Kombe la Washindi
, lilianza mwaka 1960 na lilimezwa na kombe la UEFA mwaka 1999.
Kombe la UEFA Super
, ambalo huweka pamoja washindi wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya washindi wa ligi ya UEFA Europa (awali washindi wa Kombe la Washindi), lilizinduliwa mwaka wa 1973.
Kombe la UEFA
la
Intertoto
lilikuwa ni shindano la majira ya joto, awali liliendeshwa na shirikisho la vyama vya soka vya
Uropa ya Katikati
, ambalo lilizinduliwa tena na kutambuliwa kama shindano rasmi la UEFA na UEFA mwakani 1995. Kombe la mwisho la Intertoto lilifanyika mwaka 2008. UEFA pia huandaa
Ligi ya Mabingwa ya Wanawake ya UEFA
ya vilabu vya timu za wanawake, iliyofanyika kwanza mwaka 2001, na ikajulikana kama Kombe la Wanawake la UEFA hadi 2009.
Kombe la
UEFA / CONMEBOL la inta-kontineneti
liliandaliwa pamoja na
CONMEBOL
kati ya
Ligi
ya
Mabingwa
na washindi wa
Copa Libertadores
.
Timu tatu
[2]
[3]
(Juventus, Ajax
na
Bayern Munich)
, ndio
tu zimeshinda kila shindano ya mashindano yote matatu
(Kombe la Uropa/Ligi ya Mabingwa ya UEFA, Kombe la Washindi la UEFA na Kombe la UEFA/ Ligi ya Europa),
[4]
ufanifu ambao hauna uwezekano tena kwa timu yoyote ambayo haikushinda Kombe la Washindi (kama vile Real Madrid). Kwa sasa kuna timu tisa barani Uropa ambazo zimeshinda vikombe viwili kati ya vikombe vyote vitatu; zote zimeshinda Kombe la Washindi, nne zinahitaji kushinda katika Ligi ya Mabingwa na tano zinahitaji kushinda Ligi ya Europa ya UEFA.
Juventus
ndiyo timu ya pekee barani Uropa kuwahi kushinda vikombe na michuano yote rasmi ya UEFA
[1]
na, kama upande wa kwanza katika historia ya soka ya Ulaya kuwahi kushinda mashindano matatu makuu ya UEFA, walipokea
Plaque ya UEFA
kutoka kwa Umoja wa Ulaya wa Vyama vya Mpira mnamo tarehe 12 Julai 1988
[5]
[6]
Katika futsal kuna
Futsal UEFA Cup
.
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Viungo
|
---|
|
---|
| Asia
| | |
---|
Africa
| |
---|
North,
Central America
and Caribbean
| |
---|
South America
| |
---|
Oceania
| |
---|
Europe
| |
---|
Non-FIFA
| |
---|
Games
| |
---|
|
|
---|
| Asia
| | |
---|
Africa
| |
---|
North America,
Central America
and Caribbean
| |
---|
South America
| |
---|
Oceania
| |
---|
Europe
| |
---|
Non-FIFA
| |
---|
Games
| |
---|
|
|
---|
| Asia
| | |
---|
Africa
| |
---|
Europe
| |
---|
North,
Central America
and the Caribbean
| |
---|
Oceania
| |
---|
South America
| |
---|
|
---|
National leagues
| |
---|
No national league
| Armenia
·
Andorra
·
Liechtenstein
·
Montenegro
·
San Marino
|
---|
Former leagues
| |
---|
|
---|
| Asia
| | |
---|
Africa
| |
---|
North America
Central America
and Caribbean
| |
---|
South America
| |
---|
Oceania
| |
---|
Europe
| |
---|
| |
|
---|
| Asia
| | |
---|
Africa
| |
---|
North America
Central America
and Caribbean
| |
---|
South America
| |
---|
Oceania
| |
---|
Europe
| |
---|
| |
|