한국   대만   중국   일본 
Salamu Maria - Wikipedia, kamusi elezo huru Nenda kwa yaliyomo

Salamu Maria

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kupasha Habari , kadiri ya Fra Angelico .

Salamu Maria (kwa Kilatini Ave Maria ) kwa asili ni sala ya Wakatoliki wa Kanisa la Kilatini ambayo inamsifu Bikira Maria na kumuomba sala zake hadi saa ya kufa .

Sala hiyo imeenea hata kwa Wakristo wengine, hasa Waanglikana , lakini kwa namna tofauti inatumiwa pia katika Ukristo wa Mashariki .

Hii ni kwa sababu sehemu kubwa ya sala hiyo inatokana na Injili ( Lk 1:28,42) moja kwa moja:

  • Χα?ρε, κεχαριτωμ?νη, ? Κ?ριο? μετ? σο? / Chaire, kecharit?men?, o Kyrios meta sou / Salamu uliyejaa neema, Bwana yu nawe (maneno ya Malaika Gabrieli )
  • Ε?λογημ?νη σ? ?ν γυναιξ?ν κα? ε?λογημ?νο? ? καρπ?? τ?? κοιλ?α? σου / eulog?men? su en gynaixin kai eulog?menos o karpos t?s koilias sou / Umebarikiwa wewe kati ya wanawake na umebarikiwa mzao wa tumbo lako (maneno ya Elizabeti )

Katikati ya karne ya 13 sala ilikuwa inaundwa na maneno hayo tu pamoja na kuingiza jina la Maria , inavyoonekana katika ufafanuzi wa Thoma wa Akwino . [1]

Mwishoni mwa karne ya 15 yaliongezwa maneno ya kumuomba Maria sala zake. [2]

Hatimaye sala kwa Kilatini imekuwa hivi:

Ave Maria, gratia plena,
Dominus tecum.
Benedicta tu in mulieribus,
et benedictus fructus ventris tui, Iesus. [3]
Sancta Maria, Mater Dei,
ora pro nobis peccatoribus,
nunc et in hora mortis nostrae. Amen.

Tafsiri ya Kiswahili ni:

Salamu Maria, umejaa neema,
Bwana yu nawe.
Umebarikiwa kuliko wanawake wote,
na Yesu, mzao wa tumbo lako, amebarikiwa.
Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu,
utuombee sisi wakosefu,
sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

Tanbihi [ hariri | hariri chanzo ]

  1. " "Saint Thomas Aquinas on the Hail Mary", Catholic Dossier , May-June 1996, Ignatius Press, Snohomish, Washington" . Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2015-09-24 . Iliwekwa mnamo 2015-11-07 .
  2. British Library - Rare Books Department, shelfmark: IA 27542
  3. With Pope John XXIII 's edition of the Roman Missal , the use of the letter J in printing Latin was dropped even in liturgical books, which had preserved that usage long after it ceased in the printing of ordinary Latin texts, including documents of the Holy See.

Viungo vya nje [ hariri | hariri chanzo ]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu .
Je, unajua kitu kuhusu Salamu Maria kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari .