Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mwanga wa Jua
(au
nuru ya Jua
; kwa
Kiingereza
sunlight
au
sunshine
) ni
mionzi
kwa
umbo
la
nuru inayoonekana
, nuru ya
infraredi
na
urujuanimno
ambayo hutolewa na
Jua
. Mionzi hiyo ni sehemu za
mnururisho wa sumakuumeme
unaotoka kwenye Jua.
Kwenye
Dunia
,
mwanga
wa Jua huchujwa kupitia
anga
la Dunia na ni dhahiri kwamba
mchana
, wakati Jua lipo juu ya
upeo wa macho
, mionzi ya Jua inatufikia moja kwa moja kama mchanganyiko wa nuru ya kuangaza na kuleta
joto
. Wakati anga linafunikwa na
mawingu
, mwanga wa Jua unatawanyika.
Mwanga wa Jua huchukua
muda
wa
dakika
8.3 kufikia Dunia kutoka kwenye uso wa Jua.
Upande wa
afya
mionzi ya Jua ina madhara lakini pia
faida
, kwa kuwa ni chanzo kikuu cha
vitamini D3
.
Tena mwanga wa Jua ni muhimu katika
usanisinuru
, mchakato unaotumiwa na
mimea
na
viumbehai
vingine vya
jamii
hiyo kubadili
nishati
ya mwanga, kuwa ndani ya nishati ya
kemikali
ambayo inaweza kutumika kwa kuchochea shughuli za viumbe.
Mwanga wa Jua huweza kupimwa kwa kutumia
kifaa
kinachoitwa
Kipimajua
(kwa Kiingereza: sunshine recorder, pyranometa).
|
Makala hii kuhusu mambo ya
fizikia
bado ni
mbegu
.
Je, unajua kitu kuhusu
Mwanga wa Jua
kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa
kuihariri na kuongeza habari
.
|