한국   대만   중국   일본 
Mkoa wa Sistan na Baluchistan - Wikipedia, kamusi elezo huru Nenda kwa yaliyomo

Mkoa wa Sistan na Baluchistan

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa mkoa wa Sistan na Baluchistan katika Uajemi

Sistan na Baluchistan ( kaj ??????? ? ?????????) ni moja wa mikoa 30 ya Uajemi . Makao makuu yako mjini Zahedan .

Mwaka 2006 idadi ya wakazi ilikuwa watu 2,405,742. Mkoa una eneo la 181,785 km² na msongamano wa wakazi 13 kila kilomita ya mraba.

Jiografia [ hariri | hariri chanzo ]

Mkoa uko katika kusini mashariki ya Uajemi ukipakana na Afghanistan , Pakistan , Ghuba ya Omani ( Bahari Hindi ) na mikoa jirani ya Khorasan Kusini , Kerman na Hormozgan .

Zahedan yenye wakazi 567,449 (sensa 2006) ni mji mkubwa mkoani. Kaskazini ya mkoa ni eneo la Sistan na kusini ya mkoa ni sehemu ya kiajemi ya Baluchistan .

Mkoa hupokea mvua kidogo kwa wastani milimita 80 kwa mwaka. Sehemu kubwa ya usimbishaji hupatikana kati ya Oktoba na Machi ( mvua milimita 8 - 15) na miezi kati ya Aprili na Septemba ni yabisi yenye usimbishaji wa milimita 0 - 8 pekee.

Halijoto ya wastani ni sentigredi 20.8; mwezi baridi ni Januari yenye wastani ya 7.5 °C na mwezi wa joto ni Julai yenye wastani ya 33.1 °C.

Utawala [ hariri | hariri chanzo ]

Sistan na Baluchistan huwa na wilaya 8 ambazo ni

Wakazi [ hariri | hariri chanzo ]

Wakazi walio wengi sana ni Wabaluchi ambao ni jamii kubwa yenye lugha ya pamoja wanaokalia sehemu za Uajemi mashariki, Afghanistan kusini na kusini-magharibi ya Pakistan.

Wengi wao ni Wasunni tofauti na wakazi wengine wa Uajemi walio Washia hasa.

Umaskini ni kubwa mkoani ingawa kuna malighafi kama madini mbalimbali ambazo hazikuanza kuchimbwa bado.