Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Katekisimu ya Kanisa Katoliki
(kwa kifupi
KKK
) ni kitabu rasmi cha kufundishia dini ya
Ukristo
kadiri ya
imani
na
maadili
ya
Kanisa Katoliki
kutokana na
Mtaguso wa pili wa Vatikano
.
Ilikubaliwa na
Papa Yohane Paulo II
kwanza tarehe
11 Oktoba
1992
, halafu moja kwa moja
15 Agosti
1997
.
Katika
mtandao
inapatikana katika lugha zifuatazo:
Vitabu vya kufundishia
dini
ya Kikristo vilitolewa kuanzia
Mababu wa Kanisa
, lakini neno maalumu
katekisimu
lilianza kutumiwa na
Martin Luther
mwaka
1529
.
Wakati wa
Mtaguso wa Trento
ilitolewa katekisimu kwa ajili ya ma
paroko
ili waweze kufundisha vizuri imani katoliki.
Katekisimu ya Trento
ilipitishwa na
Papa Pius V
ikaenea katika Kanisa Katoliki lote.
Baada yake, hakukuwa na katekisimu nyingine ya kimataifa, ingawa kuanzia mwaka
1905
ilienea sana ile iliyoandikwa na
Papa Pius X
kwa
jimbo
la
Roma
.
Katekisimu ya Kanisa Katoliki inatarajiwa kutumika hasa kama msingi kwa utunzi wa katekisimu za kila lugha na aina kadiri ya mahitaji ya watu.
Katekisimu ya Kanisa Katoliki ina sehemu kuu nne:
Mafundisho yote yanaendana na madondoo mengi, hasa ya
Biblia
,
Mababu wa Kanisa
,
Mitaguso ya kiekumene
, Ma
papa
na
watakatifu
.
Papa Benedikto XVI
, ambaye alipokuwa
kardinali
(Joseph Ratzinger) aliongoza utunzi wa KKK, mwaka
2005
alitoa
Ufupisho
wake, uliotafsiriwa katika
Kiswahili
kwa jina la
Ufupisho Makini
.
Katika mtandao anapatikana kwa lugha mbalimbali, k. mf. kwa Kiingereza:
Compendium of the Catechism of the Catholic Church